.

.

TUMIA VIDOLE

TUMIA VIDOLE
PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918 PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918sundwa.Blogspot.com

Tuesday, July 14, 2015

UCHAMBUZI: Nchi imejaa vijana wacheza kamari, tuwanusuru



Natambua kuwa kwa sababu mbalimbali,  walengwa husika wa  makala haya hawatosoma mawazo yangu, lakini wewe utakayebahatika kunisoma kwa pamoja, mimi na wewe tuna dhima ya kuwanusuru vijana  wa Taifa hili.

Sote ni mashahidi wa hali ya vijana wengi mjini na vijijini, vijana wanasikitisha; hawana mwelekeo na hawajielewi.

Katika Taifa lenye kila aina ya rasilimali, vijana wakiwamo wasomi wanashindwa kuzichangamkia. Wamebaki kuwa walalamikaji. Wengi wanasuburi ajira kama vile zinaletwa katika mfuko.

Kibaya zaidi wale waliotarajiwa kuwapa ajira hizo au pengine kuwajengea mazingira ya kuhimili vishindo vya maisha, wamewatosa. Wanajali matumbo yao na familia zao.

Wamebaki kuwatungia sera na kuanzisha mipango ya kudunisha vipawa na elimu yao, ilhali wao wanasomesha watoto wao  nje ya nchi kwenye elimu inayowawezesha kukabiliana na changamoto za dunia ya kileo.

Matokeo ya kususwa kwa vijana wa nchi hii kila mwenye akili timamu anayaona. Vijana wamejaa vijiweni hawajui leo wala kesho yao. Hata wanapobahatika kutia kitu mfukoni wanaishia kupeleka katika michezo ya kamari.

Leo vijana wengi wamekumbwa na pepo la  ‘kubet’ (kubashiri michezo ya mpira wa miguu). Mwelekeo na mawazo ya kupambana na maisha vimeelekezwa katika kubashiri mipira na aina nyingine za michezo ya  kamari badala ya kazi.

Kuna mwanasiasa mmoja amewahi kusema vijana wasio na ajira ni bomu linaloweza kulipuka muda wowote. Kabla halijalipuka mimi na wewe angalau tufanye kitu; tuwasaidie vijana baada ya kutoswa na wenye haki zaidi ya kufaidi matunda ya nchi hii.

Tufanyeje? Kwa kuanzia vijana hawa hawahitaji mitaji, kwani kwa namna walivyovurugwa, nina wasiwasi kuwa wanaweza kutapanya mitaji hiyo. Tuwape elimu ya kujitambua kwanza, wayajue maisha na wajibu wao katika kupambana na changamoto zake.

Tuwajenge wabadili mtazamo kuwa maisha bora hayapatikani kwa ‘kuyakatia denge’. Waelezwe ukweli kuhusu kanuni za maisha kuwa mafanikio ya kweli hayatokani na njia za mkato. Wajue kuwa dunia ina watu wachache mno waliowahi kutoka  kimaisha kwa kupitia mgongo wa  kamari.

Badala ya kuwaacha waendelee kulalamika wakiisubiri Tanzania ya asali na maziwa  ambayo haipo kwao isipokuwa kwa wateule wachache, tuwaeleze wabadili fikra kuwa maisha yanawezekana tena popote. Tena jambo zuri ni kuwa wenyewe wana msemo wao siku hizi usemao: kambi popote.

Tuwaeleze kuwa hakuna mwanasiasa mwenye dhamira ya kuwatoa kimaisha, zaidi ya kuwatumia kama  daraja  la kuwawezesha viongozi wa kisiasa kutimiza matakwa yao binafsi.

No comments:

Post a Comment