.

.

TUMIA VIDOLE

TUMIA VIDOLE
PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918 PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918sundwa.Blogspot.com

Monday, July 13, 2015

Serikali yaombwa kupeleka chakula cha msaada Butiama Mkoani Mara.


BUTIHAMA MARA:

Wananchi wa wilaya ya Butiama Mkoani Mara wanakabiliwa na  njaa kali hivyo wameiomba   serikali kuchukua hatua za haraka za kupeleka chakula cha msaada katika kunusuru maisha  ya watu ambayo sasa imesababisha baadhi ya familia kuishi kwa kunywa uji.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara ambao umeitishwa na mbunge wa jimbo hilo la Musoma Vijijini,wananchi wa kata ya Mugango na vijiji jirani katika wilaya ya butiama,wamesema  eneo hilo hivi sasa linakabiliwa na njaa kali hivyo kunahitaji msaada  wa haraka wa  chakula ili kuokoa maisha ya wananchi.
 
Hata hivyo mbunge wa jimbo la Musoma vijiji Mh. Nimrod Mkono,amekiri  wilaya hiyo kukabiliwa  na njaa kali na kusema tayari amewasiliana  na ofisi ya waziri Mkuu kwa  ajili ya kuona namna ya kutoa msaada wa haraka wa chakula katika kukabiliana na njaa  hiyo.
 
Hivi karibuni  mkuu wa mkoa wa mara Kapt.Mstaafu Asseri  Msangi  kwa  nyakati  tofauti amemweeleza waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda na makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal kuwa mkoa wa mara unakabiliwa na njaa kali,ambayo amesema imetoka na ukame  pamoja na zao la  muhogo kushambuliwa na ugonjwa wa batoto kali hivyo kuhitaji haraka tani zaidi ya elfu  kumi za 
chakula.







No comments:

Post a Comment