.

.

TUMIA VIDOLE

TUMIA VIDOLE
PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918 PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918sundwa.Blogspot.com

Wednesday, July 15, 2015

ARSENAL YAPATA PIGO JUU YA NYOTA HUYU WA URENO….

William 1
Dili la Arsenal kumsajili nyota kutoka klabu ya Spoting Lisbon ya Ureno William Carvalho limeota mbawa baada ya kiungo huyo kuumia na atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki 10 hadi 12 sawa miezi mitatu.

Carvalho ambaye mara kwa mara amekuwa akihusishwa kusajiliwa na Arsenal atakuwa nje kwa miezi michache ijayo ya msimu unaokuja baada ya kuvunjika kwa mfupa unaoitwa ‘tibia’.

WilliamMchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alikuwa ni sehemu muhimu kwenye kikosi cha Ureno chini ya miaka 21 kwenye michuano ya European Championship ambapo alitajwa kama mchezaji bora wa mashindano baada ya kuonesha kiwango cha hali ya juu kwnye mechi dhidi ya Jamhuri ya Czech.

William 2Mwanzoni Manchester United walionesha nia ya kumtaka mchezaji huyo kabla ya kubadili mipango yao na kwenda kwa viungo Morgan Schneiderling na Bastian Schweinsteiger.

No comments:

Post a Comment