.

.

TUMIA VIDOLE

TUMIA VIDOLE
PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918 PATA HABARI MBALI MBALI KUTOKA KATIKA BLOG HII PIA TANGAZA AU TOA MAONI KUPITIA Email:Luzunhowhiser@gmail.com OR Cell: 0653394330 OR 0755560918sundwa.Blogspot.com

Wednesday, July 15, 2015

Ukawa hakijaeleweka

Dar es Salaam. Mambo yamekuwa mazito. Ndivyo inavyoonekana baada ya vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kushindwa kutangaza mgombea urais jana badala yake ukatoa ahadi mpya kwamba sasa atatangazwa muda wowote ndani ya siku saba.

Kauli hiyo inayoibua maswali mengi imekuja baada ya viongozi wa umoja huo waliofanya vikao hadi usiku jana bila ya viongozi wakuu wa CUF ambao wameahidi kutoa msimamo wao leo saa 5.00 asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao hicho kilichodumu kwa saa 11.30, Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia alisema wamekamilisha mazungumzo ya kumpata mgombea wa urais ambaye watamtangaza kwenye mkutano wa hadhara muda wowote ndani ya siku saba.

Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR – Mageuzi akizungumza akiwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, na Mwenyekiti wa NLD, Dk Emmanuel Makaidi na viongozi wengine wa vyama hivyo alisema hakuna mpasuko kama inavyodaiwa na kusisitiza kwamba bado wapo na CUF katika umoja huo.

Mwenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba, Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na naibu wake wa Bara, Magdalena Sakaya hawakuhudhuria kikao hicho kilichofanyika kuanzia saa 4.00 asubuhi kwenye Hoteli ya Colosseum jijini Dar es Salaam.

Badala yake, Sakaya aliiambia Mwananchi jana jioni kuwa CUF haikuweza kushiriki kikao hicho kwa kuwa kulikuwa na mambo ambayo hawajakubaliana ndani ya chama na kwamba kama wangemaliza mapema, wangekwenda kwenye kikao hicho.

Baadaye usiku, CUF ilituma taarifa kwa vyombo vya habari ikisema kuwa itazungumza na waandishi wa habari leo saa 5.00 asubuhi kwenye ofisi za chama hicho Dar es Salaam kutoa taarifa kuhusu Ukawa.

Kutokuwapo kwa viongozi wa CUF jana na habari kwamba chama hicho kitatoa taarifa peke yake leo, kunaweka giza nene mbele ya vyama vinavyounda Ukawa; Chadema, CUF, NCCR Mageuzi na NLD, ambavyo vilikubaliana kusimamisha mgombea mmoja kuanzia ngazi ya urais hadi udiwani.

Kutokuwapo kwa viongozi wa CUF kulisababisha Ukawa kushindwa kumtaja mgombea wake na habari ambazo zilipatikana awali, zilisema huenda vyama hivyo vikatangaza jina la chama kitakachotoa mgombea urais badala ya jina la mgombea.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zilisema hoja kubwa ilikuwa katika suala la mgombea urais, nafasi ambayo inawaniwa na Profesa Lipumba ambaye ameshachukua fomu za CUF na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa ambaye anaungwa mkono na vyama vyote vinne.

Tayari Profesa Lipumba ameshagombea urais mara nne bila ya mafanikio, wakati Dk Slaa aligombea mwaka 2010 na kushika nafasi ya pili, akiwa ameitikisa CCM iliyopoteza asilimia takriban 20 ya kura za mwaka 2005.

Sakaya alisema jana kuwa CUF haikushiriki kikao cha jana kutokana na kutoafikiana baadhi ya mambo ndani ya chama chake, ikiwa ni pamoja na suala hilo la kusimamisha mgombea mmoja wa urais kupitia Ukawa.

No comments:

Post a Comment